Uchaguzi DRC: Tshisekedi anaongoza kwa kura milioni 8.8
Felix Tshisekedi, ambaye anawania kuchaguliwa tena kama rais wa DRC, alichukua mamlaka kwa mara ya kwanza Januari 2019. / Picha: Reuters
Matokeo ya awali kutoka
uchaguzi wa Jamhuri ya Kidemokrasia ya Congo yaliyotolewa Jumatano yalionyesha
kuwa Rais aliyepo, Felix Tshisekedi, anaongoza kwa kiasi kikubwa, lakini hii
ilikuja huku upinzani ukikataa matokeo ya uchaguzi na kuandaa maandamano yaliyogeuka
kuwa ya vurugu.
Asubuhi, makumi ya polisi wa
kutuliza ghasia katika mji mkuu wa Kinshasa walizuia maandamano yaliyopangwa na
upinzani dhidi ya mchakato wa uchaguzi ambayo yalikuwa yamepigwa marufuku
kufanyika.
Baadhi ya waandamanaji walijitokeza hata hivyo – lakini maandamano hayo haraka yaligeuka kuwa vurugu
wakati waandamanaji waliporusha mawe kwa maaskari.
Wanasiasa wakuu wa upinzani
Jamhuri ya Kidemokrasia ya Congo walitoa wito wa maandamano hayo baada ya
kukataa kura ya wiki iliyopita, ambayo ilikumbwa na ucheleweshaji mkubwa
. Polisi, waandamanaji wakabiliana
Waziri wa mambo ya ndani wa Congo
Peter Kazadi alisema Jumanne kwamba maandamano hayo yatazuiwa kwa sababu
"yanalenga kuharibu mchakato wa uchaguzi."
Lakini upinzani hata hivyo
uliwahimiza wafuasi kukusanyika karibu na bunge la kitaifa na kuandamana hadi
makao makuu ya tume ya uchaguzi ya nchi hiyo.
Polisi wa kutuliza ghasia
walitumwa eneo hilo na kurusha mabomu ya machozi kwa wafuasi wa mwanasiasa wa
upinzani Martin Fayulu, ambao walikusanyika katika makao makuu ya chama chake.
Wafuasi hao walirusha mawe kwa
polisi, ambao walijibu kwa kuwarushia mawe pamoja na mabomu ya machozi.
Majeruhi
Fayulu baadae alisema kuwa
watu wasiopungua 11 walikuwa wamejeruhiwa.
Mkuu wa polisi wa Kinshasa,
Jenerali Blaise Kilimbalimba, alisema maafisa wawili walijeruhiwa.
Aliongeza kuwa kulikuwa na
watoto wadogo miongoni mwa waandamanaji -- na kwamba waandaaji wa maandamano
wataitwa kwa mahojiano.
Watu takriban milioni 44
walikuwa wamesajiliwa kupiga kura Desemba 20 katika uchaguzi wa kuchagua rais,
wabunge wa kitaifa na wa kikanda na madiwani wa manispaa.
Uongozi mkubwa wa Tshisekedi
Lakini tume ya uchaguzi
ilikumbana na ugumu wa kufikisha vifaa vya kupigia kura kwa wakati katika vituo
vya kupigia kura katika nchi kubwa na dhaifu – yenye ukubwa wa takriban Ulaya
Magharibi – na kuacha baadhi ya watu wasiweze kupiga kura.
Upigaji kura rasmi uliongezwa
kwa siku moja na hata uliendelea hadi Siku ya Krismasi katika baadhi ya maeneo
ya mbali.
Msemaji wa serikali Patrick
Muyaya alisema kwenye mitandao ya kijamii kwamba upinzani unapaswa kusubiri
kuchapishwa kwa matokeo ya awali na kuwasilisha malalamiko kuhusu mchakato wa
uchaguzi kwa Mahakama ya Katiba.
Matokeo ya awali yaliyotolewa na tume ya uchaguzi Jumatano jioni
yalionyesha Rais aliyepo madarakani Felix Tshisekedi akiwa
mbele kwa kiasi kikubwa, akiwa na takriban asilimia 79 ya kura
takriban milioni 8.8 zilizohesabiwa hadi sasa.
Mgombea mwenye umri wa miaka
60, ambaye alichukua madaraka Januari 2019 baada ya kuhamishwa kwa amani kwa
mara ya kwanza nchini humo, anagombea muhula wa pili wa miaka mitano.
Moise Katumbi, aliyekuwa gavana wa eneo la
kusini-mashariki la Katanga, ana takriban asilimia 15 ya kura zilizohesabiwa
hadi sasa.
Anafuatiwa na Fayulu,
aliyekuwa mtendaji wa kampuni ya mafuta ambaye anadai alikuwa mshindi halali wa
uchaguzi wa 2018, akiwa na takriban asilimia 3.
